16Njoni, msikie, ninyi nyote mnao mwabudu Mungu, nami nitatangaza yale yeye aliyoitendea roho yangu.
17Nilimlilia kwa kinywa changu, naye alipendezwa na ulimi wangu.
18Kama ningelikuwa na dhambi ndani ya moyo wangu, Bwana asingenisikiliza.
19Lakini Mungu hakika amesikia; amesikia sautiya kuomba kwangu.
20Atukuzwe Mungu, ambaye hakuyakataa maombi yangu wala kuweka uaminifu wa agano lake mbali nami.