Text copied!
CopyCompare
Biblia ya Kiswahili - Zaburi - Zaburi 45

Zaburi 45:6-11

Help us?
Click on verse(s) to share them!
6Kiti chako cha enzi, Mungu ni cha milele na milele; na fimbo ya haki ni fimbo ya utawala wako.
7Umeipenda haki na kuchukia uovu; kwa hiyo Mungu, Mungu wako, amekupaka mafuta ya furaha kuliko wenzako.
8Mavazi yako yote hunukia manemane, udi, na mdalasini; kukoka katika majumba ya pembe vyombo vya muziki wa nyuzi vimekufurahisha.
9Binti za wafalme ni kati ya wake zako waheshimiwa; na mkono wako wa kuume amesimama malikia aliye vaa mavazi ya dhahabu ya Ofiri.
10Sikiliza, mwanangu, tafakari na utege sikio lako; uwasahahu watu wako na watu wa nyumba ya baba yako.
11Hivyo mfalme atautamani uzuri wako; yeye ni Bwana wako; umstahi.

Read Zaburi 45Zaburi 45
Compare Zaburi 45:6-11Zaburi 45:6-11