6Kwa maana sitauamini upinde wangu, wala upanga wangu hautaniokoa.
7Bali wewe ndeye uliyetuokoa na adui zetu, na umewaaibisha wale watuchukiao.
8Katika Mungu tumefanywa kujivuna siku zote, nasi tutalishukuru jina lako milele. Selah
9Lakini sasa umetutupa na kutufedhehesha, na hauendi na majeshi yetu.
10Umetufanya kuwakimbia maadui zetu; na wale watuchukiao huchukua vitu vyetu vya thamani kwa ajili yao wenyewe.
11Umetufanya kama kondoo aliyeandaliwa kwa ajili ya chakula na umetutawanya kati ya mataifa.
12Wewe unawauza watu wako bure; kwa kufanya hivyo haukupata faida.
13Wewe umetufanya kukemewa na majirani zetu, kuchekwa, na kudhihakiwa na wale wanao tuzunguka.
14Umetufaya kituko kati ya mataifa,...