14Uache uovu na utende mema. Uitafute amani na kuiendea amani.
15Macho ya Yahwe yako kwenye haki na masikio yake huelekea kulia kwao.
16Uso wa Yahwe uko kinyume na wale watendao uovu, kuikatilia mbali kumbukumbu yao duniani.
17Wenye haki hulia na Yahwe husikia na kuwaokoa kwenye matatizo yao yote.
18Yahwe yu karibu nao waliovunjika moyo, naye huwaokoa waliogandamizwa rohoni.