3Ni nani atakaye panda mlima wa Yahwe? Ni nani atakaye simama patakatifu pake?
4Yeye ambaye ana mikono misafi na moyo safi; ambaye hajauinua uongo, na haja apa kiapo ili kudanganya.
5Yeye atapokea baraka kutoka kwa Yahwe na haki kutoka kwa Mungu wa wokovu wake.