12Mawe ya barafu na makaa ya moto yalianguka kutoka katika mwangaza kabla yake.
13Yahwe aliongea katika mbingu! Sauti ya aliye juu ilisikika.
14Yeye aliifyatua mishale yake na kuwatawanya adui zake; na radi nyingi zenye mwanga alizitawanya katika maeneo tofauti tofauti.
15Ndipo mifereji ya maji ilitokea; misingi ya dunia ikadhihirishwa kwa mlio wa pigo lako, Yahwe kwa sauti ya pumzi ya pua zako.