2Msifuni yeye, enyi malaika wake wote; msifuni yeye, majeshi ya malaika wake wote.
3Msifuni yeye, enyi jua na mwezi; msifuni yeye, nyota zote zing'aazo.
4Msifuni yeye, enyi mbingu zilizo juu zaidi na maji yaliyo juu ya anga.
5Na vilisifu jina la Yahwe, maana aliamuru, navyo vikaumbwa.
6Pia ameviimrisha milele na milele; naye alitoa amri ambayo haitabadilika.