15Sanamu za mataifa ni fedha na dhahabu, kazi ya mikono ya wanadamu.
16Sanamu hizo zina vinywa, lakini haziongei; zina macho, lakini hazioni;
17zina masikio, lakini hazisikii, wala vinywani mwao hamna pumzi.
18Wale wazitengenezao wanafanana nazo, vilevile kila anaye zitumainia.
19Enyi kizazi cha Israeli, mtukuzeni Yahwe; kizazi cha Haruni, mtukuzeni Yahwe.
20Kizazi cha Lawi, mtukuzeni Yahwe.