2“Kama asingekuwa Yahwe ambaye alikuwa upande wetu wakati watu walipoinuka dhidi yetu,
3basi wangekuwa wametumeza tungali hai hasira yao lipozidi dhidi yetu.
4Maji yangetugharikisha; mto ungetuzidia.
5Kisha maji yafurikayo yangetuzamisha.”
6Atukuzwe Yahwe, ambaye hajaruhusu tuwe mawindo kwa meno yao.