Text copied!
CopyCompare
Biblia ya Kiswahili - Zaburi - Zaburi 119

Zaburi 119:78-134

Help us?
Click on verse(s) to share them!
78Wenye kiburi na waaibishwe, maana wamenitukana; bali mimi nitayatafakari maagizo yako.
79Wale wote wanao kucha wewe na wanigeukie, wale wazijuao amri za agano lako.
80Moyo wangu uwe mkamilifu pamoja na heshima kwa sheria zako ili nisiaibike. KAPH.
81Ninazimia kwa kutamani sana kuwa wewe unaweza kuniokoa! Ninamatumaini katika neno lako.
82Macho yangu yanatamani sana kuiona ahadi yako; ni lini utanifariji mimi?
83Kwa maana nimekuwa kama kiriba katika moshi; sisahau sheria zako.
84Ni kwa muda gani gani mtumishi wako atalazimika kuyavumilia haya; ni lini utawahukumu wale wanaonitesa?
85Wenye kiburi wamenichimbia shimo, wasiotii sheria yako.
86Amri zako zote ni za kuaminika; wale watu walinitesa bila ya haki; unisaidie.
87karibu kunifanya nifikie mwisho juu ya nchi hii, lakini siyakatai maagizo yako.
88Kwa upendo wako thabiti, uniweke hai, ili niweze kuzitii amri zako. LAMEDH.
89Yahwe, neno lako linasimama milele; neno lako limefanywa imara mbinguni.
90Uaminifu wako wadumu kwa ajili ya vizazi vyote; umeiimarisha nchi, nayo inadumu.
91Vitu yote yaliendelea mpaka leo hii, kama vile ulivyosema katika amri zako za haki, maana vitu vyote ni watumishi wako.
92Kama sheria yako isingekuwa furaha yangu, ningeangamia katika mateso yangu.
93Sitayasahau kamwe maagizo yako, maana kupitia hayo umeniweka hai.
94Mimi ni wako, kwa maana ninayatafuta maagizo yao.
95Waovu hujiandaa kuniangamiza, lakini nitatafuta kuzielewa amri za agano lako.
96Nimeona kuwa kila kitu kina mipaka, lakini amri zako ni pana, zaidi ya mipaka. MEM.
97Oh ni jinsi gani naipenda sheria yako! Ni tafakari yangu mchana kutwa.
98Amri zako hunifanya mwenye hekima kuliko adui zangu, maana amri zako siku zote ziko pamoja nami.
99Ninauelewa zaidi kuliko walimu wangu wote, kwa maana ninazitafakari amri za agano lako.
100Ninaelewa kuliko wale wanaonizidi umri; hii ni kwa sababu nimeyashika maagizo yako.
101Nimeiepusha miguu yangu na kila njia ya uovu ili niweze kulitii neno lako.
102Sijaenda kinyume na amri zako za haki, kwa maana wewe umenifundisha.
103Ni jinsi gani maneno yako ni matamu kwenye majaribu yangu, naam, matamu kuliko asali kinywani mwangu!
104Kupitia maagizo yako ninapata utambuzi; kwa hiyo kila njia isiyo ya kweli.
105Neno lako ni taa ya mguu miguu yangu na mwanga wa njia yangu.
106Nimeapa na nimethibitisha, kuwa nitazitii amri za haki yako.
107Nimeteswa sana; uniweke hai, Yahwe, kama ulivyoahidi katika neno lako.
108Yahwe, tafadhali pokea dhabihu yangu ya hiari ya kinywa changu, na unifundishe amri zako za haki.
109Uhai wangu ziku zote uko mkononi mwangu, lakini bado sisahau sheria yako.
110Waovu wamenitegea mtego, lakini sijapotea mbali na maagizo yako.
111Nimezifanya amri za agano lako kama urithi wangu milele, maana hizo ni furaha ya moyo wangu.
112Moyo wangu umewekwa kuzitii sheria zako milele mpaka mwisho kabisa. SAMEKH.
113Ninawachukia watu wa kusita-sita, lakini naipenda sheria yako.
114Wewe ni ficho langu na ngao yangu; nalingoja neno lako.
115Ondokeni kwangu, ninyi mtendao uovu, ili niweze kuzitii amri za Mungu wangu.
116Uniwezeshe kwa neno lako ili niweze kuishi na nisiaibike na matumaini yangu.
117Unisaidie, nami nitakuwa salama; siki zote nitazitafakari sheria zako.
118Wewe huwakataa wale wote wapoteao mbali na sheria zako, maana watu hao ni wadanganyifu na si wakuaminika.
119Wewe huwaondoa waovu wa nchi kama takataka; kwa hiyo ninazipenda amri zako thabiti.
120Mwili wangu hutetemeka kwa hofu yako, na ninaziogopa amri za haki yako. AYIN.
121Ninafanya kilicho sahihi na haki; usiniache kwa watesi wangu.
122Uwe mdhamini wa ustawi wa mtumishi wako; usiwaache wenye kiburi wanionee.
123Macho yangu yanachoka kwa kuusubiri wokovu wako na neno lako la haki.
124Mwoneshe mtumishi wako uaminifu wa agano lako, na unifundishe sheria zako.
125Mimi ni mtumishi wako; unipe uelewa ili niweze kuzijua amri za agano lako.
126Ni wakati wa Yahwe kutenda, kwa maana watu wamevunja sheria yako.
127Hakika ninazipenda amri zako kuliko dhahabu, naam, kuliko dhahabu safi.
128Hivyo ninayafuata maagizo yako yote kwa makini, na ninachukia kila njia ya uongo. PE.
129Sheria zako ni za ajabu, ndiyo sababu ninazitii.
130Ufafanuzi wa maneno yako huleta nuru; na kumpa ufahamu mjinga.
131Ninafungua kinywa changu na kutweta, maana ninazitamani amri zako.
132Unigeukie na unihurumie, kama ufanyavyo siku zote kwa wale walipendao jina lako.
133Uziongoze hatua zangu kwa neno lako; usiruhusu dhambi yeyote initawale.
134Unikomboe dhidi ya wanadamu waonevu ili niyatii maagizo yako.

Read Zaburi 119Zaburi 119
Compare Zaburi 119:78-134Zaburi 119:78-134