55Ninalifikiria jina lako wakati wa usiku, Yahwe, na kuzishika sheria zako.
56Hili limekuwa zoezi langu kwa sababu nimeyatii maagizo yako. HETH.
57Yahwe ni sehemu yangu; nimeamua kuyatii maneno yake.
58Kwa bidii ninaomba neema yako kwa moyo wangu wote; unihurumie, kama neno lako lilivyo ahidi.
59Nilizichunguza njia zangu na kugeuzia miguu yangu kwenye amri za agano lako.
60Naharakisha na sichelewi kuzishika amri zako.
61Kamba za waovu zimenifunga; nami sijaisahau sheria yako.
62Katikati ya usiku ninaamka kukushukuru wewe kwa sababu ya amri za haki yako.
63Ninaurafiki na wale wanao kuabudu wewe, wale wote watiio maagizo yako.
64Yahwe, nchi, imejaa uaminifu wa agano lako; unifundishe sheria zako. TETH.