51Wenye kiburi wamenicheka, lakini sijaiacha sheria yako.
52Nimezitafakari amri zako za haki tangu zamani, Yahwe, nami ninajifariji mwenyewe.
53Hasira kali imenishikilia kwa sababu ya waovu wanaoikataa sheria yako.
54Sheria zako zimekuwa nyimbo zangu katika nyumba ninayoishi kwa muda.
55Ninalifikiria jina lako wakati wa usiku, Yahwe, na kuzishika sheria zako.
56Hili limekuwa zoezi langu kwa sababu nimeyatii maagizo yako. HETH.
57Yahwe ni sehemu yangu; nimeamua kuyatii maneno yake.
58Kwa bidii ninaomba neema yako kwa moyo wangu wote; unihurumie, kama neno lako lilivyo ahidi.