162Ninalifurahia neno lako kama apataye nyara nyingi.
163Ninachukia na kudharau uongo, lakini naipenda sheria yako.
164Mara saba kwa siku ninakusifu wewe kwa sababu ya amri zako za haki.
165Wana amani nyingi, waipendao sheria yako; hakuna cha kuwatia mashakani.
166Naungoja wokovu wako, Yahwe, na ninatii amri zako.
167Ninazishika amri zako thabiti, na ninazipenda sana.
168Ninayashika maagizo yako na amri zako thabiti, kwa maana unajua kila kitu nifanyacho. TAV.
169Sikia kilio changu, Yahwe; unipe uelewa wa neno lako.