Text copied!
CopyCompare
Biblia Takatifu - Luka - Luka 19

Luka 19:32-39

Help us?
Click on verse(s) to share them!
32Basi, wakaenda, wakakuta sawa kama alivyowaambia.
33Walipokuwa wanamfungua yule mwana punda, wenyewe wakawauliza, “Kwa nini mnamfungua mwana punda huyu?”
34Nao wakawajibu, “Bwana anamhitaji.”
35Basi, wakampelekea Yesu yule mwana punda. Kisha wakatandika mavazi yao juu yake wakampandisha Yesu.
36Yesu akaendelea na safari, na watu wakatandaza mavazi yao barabarani.
37Alipofika karibu na Yerusalemu, katika mteremko wa mlima wa Mizeituni, umati wote na wanafunzi wake, wakaanza kushangilia na kumtukuza Mungu kwa sauti kubwa, kwa sababu ya mambo makuu waliyoyaona;
38wakawa wanasema: “Abarikiwe Mfalme ajaye kwa jina la Bwana. Amani mbinguni, na utukufu juu mbinguni!”
39Hapo baadhi ya Mafarisayo waliokuwako katika lile kundi la watu, wakamwambia Yesu, “Mwalimu, wanyamazishe wanafunzi wako!”

Read Luka 19Luka 19
Compare Luka 19:32-39Luka 19:32-39