17Hii ndiyo sababu Baba ananipenda: Niutoe uhai wangu halafu niutwae tena.
18Hakuna auchukuaye kutoka kwangu, lakini mimi nautoa mwenyewe. Ninayo mamlaka ya kuutoa, na ninayo mamlaka ya kuutwaa pia. Nimelipokea agizo hili kutoka kwa Baba.”
19Mgawanyiko tena ukatokea kati ya wayahudi kwa sababu ya maneno haya.
20Wengi wao wakasema, “Ana pepo na ni kichaa. Kwa nini mnamsikiliza?”
21Wengine wakasema, “Haya siyo maneno ya mtu aliyepagawa na mapepo. Pepo linaweza kufungua macho ya kipofu?”