Text copied!
Bibles in Swahili (individual language)

Yohana 10:17-21 in Swahili (individual language)

Help us?

Yohana 10:17-21 in Biblia Takatifu

17 “Baba ananipenda kwani nautoa uhai wangu ili nipate kuupokea tena.
18 Hakuna mtu anayeninyang'anya uhai wangu; mimi na nautoa kwa hiari yangu mwenyewe. Ninao uwezo wa kuutoa na uwezo wa kuuchukua tena. Hivi ndivyo Baba alivyoniamuru nifanye.”
19 Kukawa tena na mafarakano kati ya Wayahudi kwa sababu ya maneno haya.
20 Wengi wao wakasema, “Ana pepo; tena ni mwendawazimu! Ya nini kumsikiliza?”
21 Wengine wakasema, “Haya si maneno ya mwenye pepo. Je, pepo anaweza kuyafumbua macho ya vipofu?”
Yohana 10 in Biblia Takatifu

Yohana 10:17-21 in Biblia ya Kiswahili

17 Hii ndiyo sababu Baba ananipenda: Niutoe uhai wangu halafu niutwae tena.
18 Hakuna auchukuaye kutoka kwangu, lakini mimi nautoa mwenyewe. Ninayo mamlaka ya kuutoa, na ninayo mamlaka ya kuutwaa pia. Nimelipokea agizo hili kutoka kwa Baba.”
19 Mgawanyiko tena ukatokea kati ya wayahudi kwa sababu ya maneno haya.
20 Wengi wao wakasema, “Ana pepo na ni kichaa. Kwa nini mnamsikiliza?”
21 Wengine wakasema, “Haya siyo maneno ya mtu aliyepagawa na mapepo. Pepo linaweza kufungua macho ya kipofu?”
Yohana 10 in Biblia ya Kiswahili