Text copied!
CopyCompare
Biblia Takatifu - Yohana - Yohana 10

Yohana 10:17-21

Help us?
Click on verse(s) to share them!
17“Baba ananipenda kwani nautoa uhai wangu ili nipate kuupokea tena.
18Hakuna mtu anayeninyang'anya uhai wangu; mimi na nautoa kwa hiari yangu mwenyewe. Ninao uwezo wa kuutoa na uwezo wa kuuchukua tena. Hivi ndivyo Baba alivyoniamuru nifanye.”
19Kukawa tena na mafarakano kati ya Wayahudi kwa sababu ya maneno haya.
20Wengi wao wakasema, “Ana pepo; tena ni mwendawazimu! Ya nini kumsikiliza?”
21Wengine wakasema, “Haya si maneno ya mwenye pepo. Je, pepo anaweza kuyafumbua macho ya vipofu?”

Read Yohana 10Yohana 10
Compare Yohana 10:17-21Yohana 10:17-21