2kwa sababu mioyo yao inapanga njama za vurugu na midomo ya huongea juu ya madhara.
3Kwa hekima nyumba hujengwa na kwa ufahamu huimarishwa.
4Kwa maarifa vyumba hujazwa vitu vyote vya thamani na utajiri wa kupendeza.
5Shujaa wa hekima ni imara, na mtu wa maarifa huongeza nguvu zake;
6maana kwa uongozi wa busara unaweza kufanya vita na kwa washauri wengi kuna ushindi.
7Hekima ipo juu sana kwa mpumbavu; hafumbui kinywa chake kwenye mlango.