2 kwa sababu mioyo yao inapanga njama za vurugu na midomo ya huongea juu ya madhara.
3 Kwa hekima nyumba hujengwa na kwa ufahamu huimarishwa.
4 Kwa maarifa vyumba hujazwa vitu vyote vya thamani na utajiri wa kupendeza.
5 Shujaa wa hekima ni imara, na mtu wa maarifa huongeza nguvu zake;
6 maana kwa uongozi wa busara unaweza kufanya vita na kwa washauri wengi kuna ushindi.
7 Hekima ipo juu sana kwa mpumbavu; hafumbui kinywa chake kwenye mlango.