Text copied!
CopyCompare
Biblia Takatifu - Luka - Luka 10

Luka 10:25-34

Help us?
Click on verse(s) to share them!
25Baadaye mwalimu mmoja wa Sheria alisimama akamwuliza akitaka kumtega, “Mwalimu, nifanye nini ili nipate uzima wa milele?”
26Yesu akamwuliza, “Imeandikwa nini katika Sheria? Unaelewaje?”
27Akamjibu, “Mpende Bwana Mungu wako kwa moyo wako wote, kwa roho yako yote, kwa nguvu zako zote na kwa akili yako yote. Na, mpende jirani yako kama unavyojipenda mwenyewe.”
28Yesu akawaambia, “Vema! Fanya hivyo, nawe utaishi.”
29Lakini yeye akitaka kujihakikishia kuwa mwema akamwuliza Yesu, “Na jirani yangu ni nani?”
30Yesu akamjibu, “Mtu mmoja alikuwa anashuka kutoka Yerusalemu kwenda Yeriko. Alipokuwa njiani, alivamiwa na majambazi, wakamnyang'anya mali yake na kumpiga, wakamwacha amelala pale nusu mfu.
31Kumbe, kuhani mmoja akawa anapita barabara ileile, akamwona, akapita kando.
32Hali kadhalika na Mlawi mmoja, alipofika mahali akamwona, akapita kando.
33Lakini Msamaria mmoja aliyekuwa anasafiri, alifika pale yule mtu alipokuwa, naye alipomwona, alimwonea huruma.
34Akamwendea, akamtibu majeraha yake kwa kumtia mafuta na divai; na kuyafunga halafu akampandisha juu ya punda wake akampeleka katika nyumba moja ya wageni akamuuguza.

Read Luka 10Luka 10
Compare Luka 10:25-34Luka 10:25-34