Text copied!
CopyCompare
Biblia Takatifu - Warumi - Warumi 3

Warumi 3:9-18

Help us?
Click on verse(s) to share them!
9Tuseme nini, basi? Je, sisi Wayahudi ni bora zaidi kuliko wengine? Hata kidogo! Kwa maana nimekwisha bainisha hapo mwanzoni kwamba Wayahudi na watu wa mataifa mengine wote wako chini ya utawala wa dhambi.
10Kama Maandiko Matakatifu yasemavyo: “Hakuna hata mmoja aliye mwadilifu!
11Hakuna mtu anayeelewa, wala anayemtafuta Mungu.
12Wote wamepotoka wote wamekosa; hakuna atendaye mema, hakuna hata mmoja.
13Makoo yao ni kama kaburi wazi, ndimi zao zimejaa udanganyifu, midomoni mwao mwatoka maneno yenye sumu kama ya nyoka.
14Vinywa vyao vimejaa laana chungu.
15Miguu yao iko mbioni kumwaga damu,
16popote waendapo husababisha maafa na mateso;
17njia ya amani hawaijui.
18Hawajali kabisa kumcha Mungu.”

Read Warumi 3Warumi 3
Compare Warumi 3:9-18Warumi 3:9-18