Text copied!
CopyCompare
Biblia ya Kiswahili - Mithali - Mithali 6

Mithali 6:1-13

Help us?
Click on verse(s) to share them!
1Mwanangu, kama utaweka pesa zako kuwa dhamana kwa mkopo wa jirani yako; kama ukitoa ahadi yako katika mkopo wa mtu usiyemjua,
2basi umejiwekea mtego mwenyewe na umenaswa kwa maneno ya kinywa chako.
3Mwanagu, ukinaswa kwa maneno yako mwenyewe, fanya haya ili kujiokoa, kwa kuwa umeangukia kwenye mikono ya jirani yako; nenda unyenyekee na ufanye shauri mbele ya jirani yako.
4Usiruhusu usingizi katika macho yako wala kope za macho yako kusinzia.
5Jiokoe mwenyewe kama swala kutoka katika mkono wa mwindaji, kama ndege kutoka katika mkono wa mwinda ndege.
6Wewe mtu mvivu, mwangalie mchwa, zitafakari njia zake ili kupata busara.
7Hana akida, afisa au mtawala,
8lakini huandaa chakula chake wakati wa joto na wakati wa mavuno huweka hazina ili kula baadaye.
9Ewe mtu mvivu, utalala hata lini? Wakati gani utainuka usingizini?”
10Lala kidogo, sizia kidogo, kunja mikono kupumzika kidogo” -
11ndipo umasikini wako utakapokujia kama mporaji na uhitaji wako kama askari wa vita.
12Mtu asiyefaa-mtu mwovu- huishi kwa kauli za udanganyifu wake,
13akipepesa macho yake, akiashilia kwa miguu yake na kusonta kwa videle vyake.

Read Mithali 6Mithali 6
Compare Mithali 6:1-13Mithali 6:1-13