10Hofu ya Mungu ni chanzo cha hekima na maarifa ya Mtakatifu ni ufahamu.
11Maana kwa njia yangu siku zako zitazidishwa na uzima wako utaongezewa miaka.
12Kama unahekima, unahekima kwako mwenyewe, lakini ukidharau, utaibeba peke yako.
13Mwanamke mpumbavu anakelele nyingi- hajafunzwa wala haelewi chochote.
14Anakaa kwenye mlango wa nyumba yake, kwenye kiti cha sehemu ya juu sana ya mji.
15Anawaita kwa sauti wanaopita karibu, watu wale wanaotembea wima katika njia zao.
16Wale ambao hamjafunzwa njoni hapa ndani!” anawaambia wale wasio na akili.
17“Maji ya kuiba ni matamu na mkate unaoliwa kwa siri unapendeza.”
18Lakini hajui kwamba wafu wapo pale, wageni wake wapo kwenye vina vya kuzimu.