22utembeapo, yatakuongoza; ulalapo yatakulinda, na uamkapo yatakufundisha.
23Maana amri ni taa, na mafundisho ni nuru; kinga za kuadilisha za njia ya uzima.
24Yanakulinda dhidi ya mwanamke malaya, dhidi ya maneno laini ya uzinzi.
25Moyoni mwako usiutamani uzuri wake wala usitekwe katika kope zake.
26Kulala na malaya inaweza kugharimu bei ya kipande cha mkate, lakini mke wa mtu mwingine inagharimu uzima wako wote.
27Je mtu anaweza kubeba moto katika kifua chake bila kuuguza mavazi yake?
28Je mtu anaweza kutembea juu ya makaa bila kuchomwa miguu yake?
29Ndivyo alivyo mtu alalaye na mke wa jirani yake; yule alalaye na huyo mke hatakosa adhabu.
30Watu hawawezi kumdharau mwizi kama anaiba ili kukidhi hitaji lake la njaa.
31Walakini akimatwa, atalipa mara saba ya kile alichoiba; lazima atoe kila kitu cha thamani katika nyumba yake.
32Mtu anayefanya uzinzi hana akili; hufanya hiyo kwa uharibifu wake mwenyewe.
33Anasitahili aibu na majeraha na fedheha yake haiwezi kuondolewa.
34Maana vivu humghadhibisha mtu; hatakuwa na huruma wakati wa kulipa kisasi chake.
35Ujapompa zawadi nyingi, hatakubali mbadala wa kusuruhishwa wala kulipwa.