Text copied!
CopyCompare
Biblia ya Kiswahili - Mithali - Mithali 3

Mithali 3:23-33

Help us?
Click on verse(s) to share them!
23Ndipo utatembea katika njia yako kwa usalama na mguu wako hautajikwaa;
24ulalapo hutaogopa; utakapolala, usingizi wako utakuwa mtamu.
25Usitishwe na hofu ya ghafula au uharibifu uliosababishwa na waovu unapotokea,
26kwa maana Yehova utakuwa upande wako na ataulinda mguu wako usinaswe kwenye mtego.
27Usizuie mema kwa wale wanaoyastahili, wakati utendaji upo ndani ya mamlaka yako.
28Jirani yako usimwambie, “Nenda, na uje tena, na kesho nitakupa,” wakati pesa unazo.
29Usiweke mpango wa kumdhuru jirani yako- anayeishi jirani nawe na yeye anakuamini.
30Usishindane na mtu pasipo sababu, ikiwa hajafanya chochote kukudhuru.
31Usimhusudu mtu jeuri au kuchagua njia zake zozote.
32Maana mtu mjanja ni chukizo kwa Yehova, bali humleta mtu mwaminifu kwenye tumaini lake.
33Laana ya Yehova ipo katika nyumba ya watu waovu, bali huibariki maskani ya watu wenye haki.

Read Mithali 3Mithali 3
Compare Mithali 3:23-33Mithali 3:23-33