29Usiseme, “Mimi nitamtendea kile alichonitendea; nitalipiza kwa kile alichofanya.”
30Nilikwenda jirani na shamba la mtu mvivu, nikapita kwenye shamba la mzabibu la mtu asiye na akili.
31Miiba imeota kila sehemu, ardhi ilikuwa imefunikwa kwa upupu, na ukuta wake wa mawe ulikuwa umebomoka.
32Kisha nikaliona na kufikiria juu yake; nikatazama na kupokea mafundisho.
33Kulala kidogo, kusinzia kidogo, kupumzika kwa kukunja mikono kidogo-