25Bali wenye kuwakemea waovu watakuwa na furaha na zawadi za wema zitakuja kwao.
26Anayetoa jibu la kweli hutoa busu kwenye midomo.
27Andaa kazi yako ya nje, na tayarisha kila kitu kwa ajili yako mwenyewe shambani; baada ya hapo, jenga nyumba yako.
28Usitoe ushahidi dhidi ya jirani yako bila sababu na usidanganye kwa midomo yako.
29Usiseme, “Mimi nitamtendea kile alichonitendea; nitalipiza kwa kile alichofanya.”
30Nilikwenda jirani na shamba la mtu mvivu, nikapita kwenye shamba la mzabibu la mtu asiye na akili.
31Miiba imeota kila sehemu, ardhi ilikuwa imefunikwa kwa upupu, na ukuta wake wa mawe ulikuwa umebomoka.