Text copied!
CopyCompare
Biblia ya Kiswahili - Mithali - Mithali 23

Mithali 23:27-35

Help us?
Click on verse(s) to share them!
27Maana malaya ni shimo refu, na mke wa mume mwingine ni kisima chembamba.
28Anavizia kama mnyang'anyi na huongeza idadi ya wadanganyifu miongoni mwa wanadamu.
29Nani mwenye taabu? Nani mwenye huzuni? Nani mwenye mapigano? Nani mwenye malalamiko? Nani mwenye majeraha bila sababu? Nani mwenye macho mekundu?
30Ni wale ambao huzengea kwenye mvinyo, wale wanaojaribu kuchanganya mvinyo.
31Usiutazame mvinyo ukiwa mwekundu, wakati unametameta kwenye kikombe na kutelemka kwa uraini.
32Mwisho wake unauma kama nyoka na sumu yake kama kifutu.
33Macho yako yataona vitu vigeni na moyo wako utatamka vitu vya ukaidi.
34Utakuwa kama anayelala kwenye bahari au anayelala juu ya mlingoti.
35“Wamenipiga,” utasema, “lakini sikuumia. Wamenichapa, lakini sikuwa na hisia. Nitaamka lini? Nitatafuta kinywaji kingine.”

Read Mithali 23Mithali 23
Compare Mithali 23:27-35Mithali 23:27-35