Text copied!
CopyCompare
Biblia ya Kiswahili - Mithali - Mithali 22

Mithali 22:7-16

Help us?
Click on verse(s) to share them!
7Watu matajiri huwatawala watu masikini na mwenye kukopa ni mtumwa wa yule anayekopesha.
8Yule anayepanda udhalimu atavuna taabu na fimbo ya hasira yake itanyauka.
9Mwenye jicho la ukarimu atabarikiwa, maana anashiriki mkate wake pamoja na masikini.
10Mfukuze mbali mwenye dhihaka, na ugomvi utaondoka, mashindano na matukano yatakoma.
11Anayependa moyo safi na mwenye maneno ya neema, atakuwa rafiki yake mfalme.
12Macho ya Yehova huyaangalia maarifa, bali huyapindua maneno ya wadanganyifu.
13Mtu mvivu husema, “Kuna simba mtaani! Nitauwawa sehemu za njia.”
14Kinywa cha malaya ni shimo lenye kina kirefu; hasira ya Yehova huchochewa dhidi ya yule anayetumbukia ndani yake.
15Upumbavu umefungwa katika moyo wa mtoto, lakini marudi ya fimbo huutoa.
16Anayewanyanyasa watu masikini ili kuongeza mali yake, au kuwapa matajiri, atakuwa masikini.

Read Mithali 22Mithali 22
Compare Mithali 22:7-16Mithali 22:7-16