13Mtu mvivu husema, “Kuna simba mtaani! Nitauwawa sehemu za njia.”
14Kinywa cha malaya ni shimo lenye kina kirefu; hasira ya Yehova huchochewa dhidi ya yule anayetumbukia ndani yake.
15Upumbavu umefungwa katika moyo wa mtoto, lakini marudi ya fimbo huutoa.
16Anayewanyanyasa watu masikini ili kuongeza mali yake, au kuwapa matajiri, atakuwa masikini.