Text copied!
CopyCompare
Biblia Takatifu - Luka - Luka 1

Luka 1:48-77

Help us?
Click on verse(s) to share them!
48Kwa kuwa amemwangalia kwa huruma mtumishi wake mnyenyekevu. Hivyo tangu sasa watu wote wataniita mwenye heri.
49Kwa kuwa Mwenyezi Mungu amenitendea makuu, jina lake ni takatifu.
50Huruma yake kwa watu wanaomcha hudumu kizazi hata kizazi.
51Amefanya mambo makuu kwa mkono wake: amewatawanya wenye kiburi katika mawazo ya mioyo yao;
52amewashusha wenye nguvu kutoka vitu vyao vya enzi, akawakweza wanyenyekevu.
53Wenye njaa amewashibisha mema, matajiri amewaacha waende mikono mitupu.
54Amemsaidia Israeli mtumishi wake, akikumbuka huruma yake.
55Kama alivyowaahidia wazee wetu Abrahamu na wazawa wake hata milele.”
56Maria alikaa na Elisabeti kwa muda upatao miezi mitatu, halafu akarudi nyumbani kwake.
57Wakati wa kujifungua kwake Elisabeti ulifika, akajifungua mtoto wa kiume.
58Jirani na watu wa jamaa yake walipopata habari kwamba Bwana amemwonea huruma kubwa, walifurahi pamoja naye.
59Halafu siku ya nane walifika kumtahiri mtoto, wakataka kumpa jina la baba yake, Zakariya.
60Lakini mama yake akasema, “La, sivyo, bali ataitwa Yohane.”
61Wakamwambia, “Mbona hakuna yeyote katika ukoo wake mwenye jina hilo?”
62Basi, wakamwashiria baba yake wapate kujua alitaka mtoto wake apewe jina gani.
63Naye akaomba kibao cha kuandikia, akaandika hivi: “Yohane ndilo jina lake.” Wote wakastaajabu.
64Papo hapo midomo na ulimi wake Zakariya vikafunguliwa, akawa anaongea akimsifu Mungu.
65Hofu ikawaingia jirani wote, na habari hizo zikaenea kila mahali katika milima ya Yudea.
66Wote waliosikia mambo hayo waliyatafakari mioyoni mwao wakisema: “Mtoto huyu atakuwa mtu wa namna gani?” Maana, hakika nguvu ya Bwana ilikuwa pamoja naye.
67Zakariya, baba yake mtoto, akajazwa Roho Mtakatifu, akatamka ujumbe wa Mungu:
68“Asifiwe Bwana Mungu wa Israeli, kwani amekuja kuwasaidia na kuwakomboa watu wake.
69Ametupatia Mwokozi shujaa, mzawa wa Daudi mtumishi wake.
70Aliahidi hapo kale kwa njia ya manabii wake watakatifu,
71kwamba atatuokoa mikononi mwa adui zetu na kutoka mikononi mwa wote wanaotuchukia.
72Alisema atawahurumia wazee wetu, na kukumbuka agano lake takatifu.
73Kiapo alichomwapia Abrahamu baba yetu, ni kwamba atatujalia sisi
74tukombolewe kutoka adui zetu, tupate kumtumikia bila hofu,
75kwa unyofu na uadilifu mbele yake, siku zote za maisha yetu.
76Nawe mwanangu, utaitwa, nabii wa Mungu Mkuu, utamtangulia Bwana kumtayarishia njia yake;
77kuwatangazia watu kwamba wataokolewa kwa kuondolewa dhambi zao.

Read Luka 1Luka 1
Compare Luka 1:48-77Luka 1:48-77