20Mwanangu, kwa nini uwe mateka wa malaya, kwa nini uyakumbatie matiti ya mwanamke mgeni?
21Yehova huona kila kitu afanyacho mtu na huangalia mapito yake yote.
22Mtu mwovu atatekwa na makosa yake mwenyewe; kamba za dhambi yake zitamnasa kwa nguvu.
23Atakufa kwa kukosa maonyo; atapotelea mbali kwa upumbavu wake wingi.