20 Mwanangu, kwa nini uwe mateka wa malaya, kwa nini uyakumbatie matiti ya mwanamke mgeni?
21 Yehova huona kila kitu afanyacho mtu na huangalia mapito yake yote.
22 Mtu mwovu atatekwa na makosa yake mwenyewe; kamba za dhambi yake zitamnasa kwa nguvu.
23 Atakufa kwa kukosa maonyo; atapotelea mbali kwa upumbavu wake wingi.