Text copied!
CopyCompare
Biblia ya Kiswahili - Mithali - Mithali 5

Mithali 5:12-23

Help us?
Click on verse(s) to share them!
12Nanyi mtasema, “Namna gani nilichukia fundisho na moyo wangu ulidharau sahihisho!
13Sikuweza kuwatii walimu wangu au kuwasikiliza walionielekeza.
14Nilikuwa nimeharibika kabisa katikati ya kusanyiko, miongoni mwa makutano ya watu.”
15Munywe maji kutoka kwenye birika lenu mwenyewe na munywe maji yanatiririka kutoka kwenye kisima chenu.
16Je inapaswa chemichemi yenu ifurike popote na mifereji yenu ya maji itiririke katika njia kuu?
17Yawe yenu wenyewe peke yenu wala si kwa wageni.
18Chemichemi yako ibarikiwe na umfurahie mke wa ujana wako.
19Maana ni ayala apendezaye na kulungu mwenye uzuri. Matiti yake na yakujaze furaha muda wote; daima na utekwe na upendo wake.
20Mwanangu, kwa nini uwe mateka wa malaya, kwa nini uyakumbatie matiti ya mwanamke mgeni?
21Yehova huona kila kitu afanyacho mtu na huangalia mapito yake yote.
22Mtu mwovu atatekwa na makosa yake mwenyewe; kamba za dhambi yake zitamnasa kwa nguvu.
23Atakufa kwa kukosa maonyo; atapotelea mbali kwa upumbavu wake wingi.

Read Mithali 5Mithali 5
Compare Mithali 5:12-23Mithali 5:12-23