Text copied!
Bibles in Swahili (individual language)

Mithali 5:12-23 in Swahili (individual language)

Help us?

Mithali 5:12-23 in Biblia ya Kiswahili

12 Nanyi mtasema, “Namna gani nilichukia fundisho na moyo wangu ulidharau sahihisho!
13 Sikuweza kuwatii walimu wangu au kuwasikiliza walionielekeza.
14 Nilikuwa nimeharibika kabisa katikati ya kusanyiko, miongoni mwa makutano ya watu.”
15 Munywe maji kutoka kwenye birika lenu mwenyewe na munywe maji yanatiririka kutoka kwenye kisima chenu.
16 Je inapaswa chemichemi yenu ifurike popote na mifereji yenu ya maji itiririke katika njia kuu?
17 Yawe yenu wenyewe peke yenu wala si kwa wageni.
18 Chemichemi yako ibarikiwe na umfurahie mke wa ujana wako.
19 Maana ni ayala apendezaye na kulungu mwenye uzuri. Matiti yake na yakujaze furaha muda wote; daima na utekwe na upendo wake.
20 Mwanangu, kwa nini uwe mateka wa malaya, kwa nini uyakumbatie matiti ya mwanamke mgeni?
21 Yehova huona kila kitu afanyacho mtu na huangalia mapito yake yote.
22 Mtu mwovu atatekwa na makosa yake mwenyewe; kamba za dhambi yake zitamnasa kwa nguvu.
23 Atakufa kwa kukosa maonyo; atapotelea mbali kwa upumbavu wake wingi.
Mithali 5 in Biblia ya Kiswahili