1Wanangu, sikilizeni, fundisho la baba, na zingatieni ili mjue maana ya ufahamu.
2Mimi ninawapa mafundisho mazuri; msiyaache mafundisho yangu.
3Mimi nilikuwa mwana kwa baba yangu, mpole na mtoto pekee kwa mama yangu,
4baba alinifundisha akiniambia, “Moyo wako uzingatie sana maneno yangu; shika amri zangu nawe uishi.
5Jipatie hekima na ufahamu; usisahau na kuyakataa maneno ya kinywa changu;
6usiiache hekima nayo itakulinda; ipenda nayo itakuhifadhi salama.
7Hekima ni kitu cha muhimu sana, hivyo jipatie hekima na tumia namna zote kuweza kupata ufahamu.
8Tunza hekima nayo itakutukuza; ikumbatie nayo itakuheshimu.
9Hekima itaweka kilemba cha heshima juu ya kichwa chako; itakupa taji zuri.
10Mwanangu, sikiliza, na kuzingatia maneno yangu, nawe utapata miaka mingi ya maisha yako.
11Ninakuelekeza katika njia ya hekima, nimekuongoza katika mapito yaliyonyooka.