Text copied!
CopyCompare
Biblia ya Kiswahili - Mithali - Mithali 26

Mithali 26:17-24

Help us?
Click on verse(s) to share them!
17Kama mtu anayeshikilia masikio ya mbwa, ndivyo alivyo mpitajia anayepata hasira kwenye ugomvi ambao si wake.
18Kama mtu mwendawazimu anayetupa mishale,
19ndivyo alivyo ambaye humdanganya jirani yake na kusema, “Je sikuwa naongea utani?”
20Kwa kukosa kuni, moto huzimika; na pale pasipo na mmbea ugomvi hukoma.
21Mkaa ni kwa kuwasha makaa na kuni kwa ajili ya moto, ndivyo alivyo mtu mgomvi kwa kuwasha ugomvi.
22Maneno ya mmbea ni kama chembe tamu; nazo zinashuka chini kwenye sehemu za ndani ya mwili.
23Kioo kinachofunika chombo cha udongo ni kama midomo inayoungua na moyo mbaya.
24Yule ambaye huwachukia wengine huficha hisia zake kwa midomo na hufunika uongo ndani yake mwenyewe.

Read Mithali 26Mithali 26
Compare Mithali 26:17-24Mithali 26:17-24