25Bali wenye kuwakemea waovu watakuwa na furaha na zawadi za wema zitakuja kwao.
26Anayetoa jibu la kweli hutoa busu kwenye midomo.
27Andaa kazi yako ya nje, na tayarisha kila kitu kwa ajili yako mwenyewe shambani; baada ya hapo, jenga nyumba yako.
28Usitoe ushahidi dhidi ya jirani yako bila sababu na usidanganye kwa midomo yako.