Text copied!
CopyCompare
Biblia ya Kiswahili - Mithali - Mithali 24

Mithali 24:13-23

Help us?
Click on verse(s) to share them!
13Mwanangu, kula asali kwa kuwa ni nzuri, kwa sababu matone ya sega la asali ni matamu unapoonja.
14Hekima ndiyo ilivyo katika nafsi yako - kama utaitafuta, tumaini lako halitabatilika na kutakuwa na tumaini.
15Usisubiri kwa kuvizia kama waovu ambao hushambulia nyumba ya mwenye haki. Usiiharibu nyumba yake!
16Maana mwenye haki huanguka mara saba na kuinuka tena, lakini waovu huangushwa kwa maafa.
17Usisherekee wakati adui yako anapoanguka na wala moyo wako usifurahi anapojikwaa,
18au Yehova ataona na kutoridhika na kuondoa ghadhabu juu yake.
19Usifadhaike kwa sababu ya watenda mabaya, na wala usiwahusudu watu waovu,
20maana mtu mbaya hana matumaini na taa ya watu waovu itazimika.
21Mwanangu; mche Yehova, na umwogope mfalme, usishirikiane na watu wenye kuasi dhidi yao,
22maana kwa ghafula msiba wao utakuja na ni nani ajuaye ukubwa wa uharibifu utakao kuja kutoka kwa hao wote?
23Haya ni maneno ya wenye busara pia. Upendeleo katika kuhukumu kesi kwa sheria si vizuri.

Read Mithali 24Mithali 24
Compare Mithali 24:13-23Mithali 24:13-23