Text copied!
Bibles in Swahili (individual language)

Mithali 24:13-23 in Swahili (individual language)

Help us?

Mithali 24:13-23 in Biblia ya Kiswahili

13 Mwanangu, kula asali kwa kuwa ni nzuri, kwa sababu matone ya sega la asali ni matamu unapoonja.
14 Hekima ndiyo ilivyo katika nafsi yako - kama utaitafuta, tumaini lako halitabatilika na kutakuwa na tumaini.
15 Usisubiri kwa kuvizia kama waovu ambao hushambulia nyumba ya mwenye haki. Usiiharibu nyumba yake!
16 Maana mwenye haki huanguka mara saba na kuinuka tena, lakini waovu huangushwa kwa maafa.
17 Usisherekee wakati adui yako anapoanguka na wala moyo wako usifurahi anapojikwaa,
18 au Yehova ataona na kutoridhika na kuondoa ghadhabu juu yake.
19 Usifadhaike kwa sababu ya watenda mabaya, na wala usiwahusudu watu waovu,
20 maana mtu mbaya hana matumaini na taa ya watu waovu itazimika.
21 Mwanangu; mche Yehova, na umwogope mfalme, usishirikiane na watu wenye kuasi dhidi yao,
22 maana kwa ghafula msiba wao utakuja na ni nani ajuaye ukubwa wa uharibifu utakao kuja kutoka kwa hao wote?
23 Haya ni maneno ya wenye busara pia. Upendeleo katika kuhukumu kesi kwa sheria si vizuri.
Mithali 24 in Biblia ya Kiswahili