Text copied!
CopyCompare
Biblia ya Kiswahili - Mithali - Mithali 19

Mithali 19:15-28

Help us?
Click on verse(s) to share them!
15Uvivu unamtupa mtu kwenye usingizi mzito, bali asiyetamani kufanya kazi atakwenda njaa.
16Yeye anayetii amri huyaongoza maisha yake, bali mtu asiyefikiri juu ya njia zake atakufa.
17Mwenye ukarimu kwa masikini humkopesha Yehova na atalipwa kwa kile alichofanya.
18Mrudi mwanao wakati kuna matumaini na usiwe na shauku ya kumweka katika mauti.
19Mtu mwenye hasira kali lazima alipe adhabu; kama ukimwokoa, utafanya hivyo mara mbili.
20Sikiliza ushauri na ukubali maelekezo, ili uweze kuwa na hekima mwishoni mwa maisha yako.
21Moyoni mwa mtu kuna mipango mingi, bali kusudi la Yehova ndilo litakalo simama.
22Shauku ya mtu ni uaminifu na mtu masikini ni bora kuliko muongo.
23Kumheshimu Yehova huwaelekeza watu kwenye uzima; mwenye nayo atashibishwa na hatadhurika kwa madhara.
24Mtu goigoi huuzika mkono wake ndani ya dishi; hataurudisha juu ya kinywa chake.
25Kama utampiga mwenye mzaha, wajinga watakuwa na hekima; mwelekeze mwenye ufahamu, naye atapata maarifa.
26Anayempora baba yake na kumfukuza mama yake ni mwana anayeleta aibu na shutuma.
27Mwanangu, kama utaacha kusikiliza maelekezo, utapotea kutoka kwenye maneno ya maarifa.
28Shahidi mpotofu huidhihaki haki na kinywa cha waovu humeza uovu.

Read Mithali 19Mithali 19
Compare Mithali 19:15-28Mithali 19:15-28