23Moyo wa mtu mwenye hekima hutoa busara katika kinywa chake na huongeza ushawishi katika midomo yake.
24Maneno yenye kufaa ni sega la asali -matamu kwenye nafsi na huponya mifupa.
25Kuna njia ambayo huonekana sawa kwa mtu, bali mwisho wake ni njia ya mauti.
26Hamu ya kibarua humfanyia kazi; njaa yake humsihi kuendelea.
27Mtu duni huchimba madhara na usemi wake ni kama moto unaounguza.
28Mtu mkaidi huchochea mafarakano na umbeya huwafarakanisha marafiki.