Text copied!
CopyCompare
Biblia Takatifu - Yohana - Yohana 11

Yohana 11:10-22

Help us?
Click on verse(s) to share them!
10Lakini mtu akitembea usiku atajikwaa kwa maana mwanga haumo ndani yake.”
11Yesu alipomaliza kusema maneno hayo, akawaambia, “Rafiki yetu Lazaro amelala, lakini mimi nitakwenda kumwamsha.”
12Wanafunzi wake wakamwambia, “Bwana, ikiwa amelala, basi atapona.”
13Wao walidhani kwamba alikuwa amesema juu ya kulala usingizi, kumbe alikuwa amesema juu ya kifo cha Lazaro.
14Basi, Yesu akawaambia waziwazi, “Lazaro amekufa;
15Lakini nafurahi kwa ajili yenu kwamba sikuwako huko, ili mpate kuamini. Haya, twendeni kwake.”
16Thoma (aitwaye Pacha) akawaambia wanafunzi wenzake, “Twendeni nasi tukafe pamoja naye!”
17Yesu alipofika huko alikuta Lazaro amekwisha kaa kaburini kwa siku nne.
18Kijiji cha Bethania kilikuwa karibu na Yerusalemu umbali upatao kilomita tatu.
19Wayahudi wengi walikuwa wamefika kwa Martha na Maria kuwafariji kwa kifo cha kaka yao.
20Basi, Martha aliposikia kwamba Yesu alikuwa anakuja, akaenda kumlaki; lakini Maria alibaki nyumbani.
21Martha akamwambia Yesu, “Bwana, kama ungalikuwa hapa, kaka yangu hangalikufa!
22Lakini najua kwamba hata sasa chochote utakachomwomba Mungu, atakupa.”

Read Yohana 11Yohana 11
Compare Yohana 11:10-22Yohana 11:10-22