6Sikiliza na mimi nitasema mambo mazuri na nifumbuapo midomo yangu nitaongea haki.
7Maana kinywa changu hunena uaminifu na midomo yangu huchukia uovu.
8Maneno ya kinywa changu yote ni haki; hakuna kilichogeuzwa wala kupotoshwa.
9Maneno yangu yote yamenyooka kwa yule mwenye kuelewa; maneno yangu ni haki kwa wale wanaotafuta maarifa.
10Chagua fundisho langu badala ya fedha na maarifa kuliko dhahabu safi.
11Maana mimi, hekima ni bora kuliko vito; hakuna unachokitamani kinaweza kulinganishwa na mimi.
12Mimi, hekima, naishi kwa utaratibu, na ninamiliki maarifa na busara.