Text copied!
CopyCompare
Biblia ya Kiswahili - Mithali - Mithali 8

Mithali 8:19-28

Help us?
Click on verse(s) to share them!
19Tunda langu ni bora kuliko dhahabu, bora hata kuliko dhahabu safi.
20Ninazalisha kilicho bora kuliko fedha safi. Natembea katika njia ya haki,
21katika mapito ambayo huelekea kwenye haki, ili niwape urithi wale wanaonipenda na kuzijaza hazina zao.
22Yehova aliniumba tokea mwanzo- mwazoni mwa matendo yake ya nyakati za kale.
23Tokea enzi za kale niliwekwa katika nafasi- tokea kwanza, tokea mwanzo wa dunia.
24Kabla ya bahari, mimi nilizaliwa- kabla ya kuwepo chemchemi zenye maji tele.
25Kabla ya milima na vilima kuwekwa, mimi nilizaliwa.
26Nilizaliwa kabla ya Yehova hajaiumba dunia wala makonde, hata mavumbi ya kwanza katika dunia.
27Nilikuwepo alipoziimarisha mbingu, wakati alipochora mstari katika sura ya kilindi.
28Nilikuwepo alipoimarisha anga la juu na wakati wa kutengeneza kina cha chemchemi.

Read Mithali 8Mithali 8
Compare Mithali 8:19-28Mithali 8:19-28