17Kitanda changu nimenyunyizia manemane, udi na mdalasini.
18Njoo, tunywe tujishibishe kwa upendo wetu hata asubuhi; tupate furaha kuu kwa matendo ya mahaba.
19Maana mume wangu hayupo nyumbani kwake; amekwenda safari ya mbali.
20Alichukua mkoba wa fedha; atarudi siku ya mwezi mpevu.
21katika maneno yake mengi akamshinda; na kwa midomo yake laini anampotosha.
22Ghafula alimfuata kama maksai anayekwenda kwa mchinjaji, kama ayala aliyekamatwa kwa nguvu,
23mpaka mshale upasue ini lake. Alikuwa kama ndege anayekimbili kwenye mtego. Hakujua kuwa itamgharimu maisha yake.
24Na sasa, wanangu, nisikilizeni; zingatieni maneno ya kinywa changu.
25Moyo wako usiyageukie mapito yake; usipotoshwe katika mapito yake.