Text copied!
CopyCompare
Biblia ya Kiswahili - Mithali - Mithali 6

Mithali 6:6-13

Help us?
Click on verse(s) to share them!
6Wewe mtu mvivu, mwangalie mchwa, zitafakari njia zake ili kupata busara.
7Hana akida, afisa au mtawala,
8lakini huandaa chakula chake wakati wa joto na wakati wa mavuno huweka hazina ili kula baadaye.
9Ewe mtu mvivu, utalala hata lini? Wakati gani utainuka usingizini?”
10Lala kidogo, sizia kidogo, kunja mikono kupumzika kidogo” -
11ndipo umasikini wako utakapokujia kama mporaji na uhitaji wako kama askari wa vita.
12Mtu asiyefaa-mtu mwovu- huishi kwa kauli za udanganyifu wake,
13akipepesa macho yake, akiashilia kwa miguu yake na kusonta kwa videle vyake.

Read Mithali 6Mithali 6
Compare Mithali 6:6-13Mithali 6:6-13