27Je mtu anaweza kubeba moto katika kifua chake bila kuuguza mavazi yake?
28Je mtu anaweza kutembea juu ya makaa bila kuchomwa miguu yake?
29Ndivyo alivyo mtu alalaye na mke wa jirani yake; yule alalaye na huyo mke hatakosa adhabu.
30Watu hawawezi kumdharau mwizi kama anaiba ili kukidhi hitaji lake la njaa.
31Walakini akimatwa, atalipa mara saba ya kile alichoiba; lazima atoe kila kitu cha thamani katika nyumba yake.
32Mtu anayefanya uzinzi hana akili; hufanya hiyo kwa uharibifu wake mwenyewe.
33Anasitahili aibu na majeraha na fedheha yake haiwezi kuondolewa.