7Sasa, wanangu, nisikilizeni; wala msiache kusikiliza maneno ya kinywa changu.
8Lindeni njia yenu mbali naye wala msiende karibu na mlango wa nyumba yake.
9Kwa njia hiyo hamtawapa wengine heshima yenu au miaka ya uzima wenu kwa mtu mkatiri;
10wageni usije kufanya karamu kwa utajiri wenu; kazi mliyoifanya haitaenda katika nyumba ya wageni.