13Shika mwongozo wala usiuache, utakuongoza, maana ni uzima wako.
14Usifuate njia ya waovu wala usiende katika njia ya watendao uovu.
15Jiepushe nayo, usipite katika njia hiyo; geuka na upite njia nyingine.
16Maana hawawezi kulala mpaka wafanye ubaya na hupotewa na usingizi hadi wasababishe mtu kujikwaa.
17Maana wao hula mkate wa uovu na hunywa divai ya vurugu.